Sura 2

1 Lakini weye sema yenye inastahili na mafundisho mazuri. 2 Bazee banapashwa kuwa bapole, bakuheshimiwa, bakamilifu katika imani, mapendo na uvumilivu. 3 Vile vile, bamama bazee bana pashwa kutembeya sawa baheshimiwa, basikuwe batu ba kusingiziana. Basikuwe balevi. Bana pashwa kufundisha maneno mazuri; 4 Kusudi bafundishe biyana banamuke kupenda babwana na batoto yabo. 5 Banapashwa kubafundisha kuwa na akili, basafi, kufanya kazi ya nyumba yabo, baheshimiye babwana yabo.Kusudi neno ya Mungu isizaraulike. 6 Vile vile, unapashwa kushauriya biyana bakuwe na akili. 7 Mu byote; unapashwa kuwa mufano kwa matendo mazuri, na kama una fundisha, onyesha ukamilifu na heshima. 8 Tangaza habari safi bila kulaumiwa, kusudi mwenye ubishi apate haya sababu akuna mabaya ndani yetu. 9 Batumwa banapashwa kuheshimiya ba afande yabo. Banapashwa kubafurahisha lakini basifanye nabo ubishi. 10 Basikuwe bajanja lakini bakuwe baaminifu, kusudi baheshimiye mafundisho yetu kuhusu Mungu. Mwokozi wetu. 11 Sababu neema ya Mungu ilionekana kwa batu bote. 12 Ina tufundisha tukatale zambi na tamaa za dunia, tuishi na akili, tuwe sawa, safi katika siku za leo. 13 Wakati tunachunga kupokeya baraka yenye tunatumainia, kuonekana ya utukufu wa Mungu Mukubwa na Bwana wetu Yesu Kristu. 14 Yesu ye peke alijitowa ju yetu kusudi atukombowe na uasi yote na kuji safishia taifa yenye kuwa na kiwu ya matendo mazuri. 15 Sema na ubape moyo ju ya ile mambo. Hamakia sawa vile Mukubwa, hata mutu moya asikuzarau.