1 Ubakumbushe kujishusha mbele ya biongozi na bakubwa, babaheshimiye na kukuwa tayari kwa kazi yote ya muzuri. 2 Basitukane mutu baepuke mabishano, baheshimie bengine, na kujishusha mbele ya batu bote. 3 Sababu na shiye, tulikwaka bagumu na bakosa adabu, bapotevu na batumwa ba kila tamaa na furaha ya dunia. Tuliishi mu mabaya na tamaa, tulikuwa bakukataliwa na kuchukiyana shiye benyewe. 4 Wakati bwema bwa Mungu Mwokozi wetu na mapendo yake kwa batu ilionekana, 5 Alitokoa, haiko juu tulifanya matendo ya haki, lakini ni kwa rehema yake. Pia ilikuwa kupitia ubatizo na kuzaliwa mara ya pili kwa nguvu ya Roho Mutakatifu. 6 Kupitia Yesu Kristo Mwokozi wetu, Mungu alitumwangiya Roho Mutakatifu kwa uwingi. 7 Akaifanya kusudi tukishuhudiwa kwa neema yake, tukuwe bariti kupitia tumaini ya uzima wa milele. 8 Hii habari inastahili kuaminiwa. Nataka useme na uhakika kuhusu hii maneno, kusudi benye banaamini Mungu bajitowe kwa matendo mazuri yenye aliweka mbele yabo. Ibi byote ni bizuri na byalazima kwa batu bote. 9 Lakini, epuka mabishano ya bujinga, ya bizazi, magonvi na matengano juu ya sheriya. Ni bitu byenye abina maana wala faida. 10 Mutu yote wakuleta mugawanyiko, ukimukataza mara pili, kama hakusikiye, jitenge naye. 11 Na ujuwe kama mutu wa vile, alisha jitosha munjia ya sawa, iko na fanya zambi na kujihukumu ye peke. 12 Wakati nita kutumiya Artemasi ao Tikiko, fanya haraka unikute Nikopole, kwenye niliamuwa kubakiya wakati ya baridi kali. 13 Unitumiye Zenasi mwenye kujua sheria na Apolo, basikose hata kitu moya. 14 Batu yetu banapashwa kujifunza kufanya kazi, kusudi basikose kitu ya kusaidiya kama kuko maitaji, basikose kuzaa matunda. 15 Benye niko nabo bote banakusalimiya. Usalimiye bote benye kutupenda katika imani. Neema ikuwe kwenu nyie bote.