1 Paulo mtumishi wa Mungu na mtume wa Yesu Kristo kwa imani ya ba chaguliwa ba Mungu na ujuzi wa ukweli yenyi kupatana na kueshimu maneno ya Mungu. 2 Musimamo yaile iko juya kitumaini ya maisha ya milele ya Mungu, huyu hasemake bongo, alibalaganishaka tangia zamani. 3 Kuko wakati alionyesha neno lake waziwazi kwa mahubiri yenye alinipa nihubiri . Nilipashua kuifanya kwa amri ya Mungu mukombozi wetu. 4 KwakoTito mutoto wangu wa kweli ndani ya imani. Neema na amani kutoka kwa Mungu Baba na kwa Yesu Kristo Mkombozi wetu. 5 Juu ya ile njo nilikuacha Creti, utengeneze mambo yenye ilibakiaka, na uweke bazee ndani ya kila muji kufuatana na amri zangu. 6 Mzee anapashwa kuwa sawa, akue na mwanamuke moya tu, batoto yake bakuwe baaminifu, basi shitakiwe kuwa babaya wala bakosa adabu. 7 Mzee kama vile muchungaji wa nyumba ya Mungu, asikuwe mwenye makosa, hapashwe kuwa na masemi mabaya wala kiburi. Hapashwe kuwa mutu wa kusirika na asikuwe mulevi. Asikuwe mutu wakutomboka wala wa tamaa. 8 Lakini anapashwa kukaribisha batu, rafiki ya batu bazuri, anapashwa kuwa mwepesi, sawa, mtakatifu, na kujangaliya. 9 Anapashwa kukamatana na neno ya kweli gisi ilifundishiwa. Akuwe pia mutu wa kupatia bengine moyo kupitia mafundisho mazuri, na kurudisha bapinzani mu njiya. 10 Kwa sababu, mu bale benye balitahiriwa kuko baasi ba mingi. Maneno yabo haina maana. Bana vunja batu moyo na ku bapoteza. 11 Ni lazima kuwasimamisha. Juu ya faida yabo ya haya, banafundisha byenye habistahili na bana haribisha ma jamaa. 12 Mutu moya wa hekima kati yabo alisema: «Wakreti ni banasema bongo, batu babaya biko sawa nyama ya hatari tena bavivu.» 13 Ni ushuhuda ya kweli, ubakaripiye kabisa bakuwe na imani ya kweli. 14 Mujitshunge na mafundisho ya bayahudi na amri ya kutosha batu ndani ya kweli. 15 Kwa batakatifu byote ni safi. Lakini kwa bachafu na benye haba amini hakuna kisafi. Sababu mawazo na zamiri yabo ilichafuliwa. 16 Banasema kama banajua Mungu, lakini matendo yabo ni tofauti. Habastahili ushuhuda muzuri, ni baasi.