Sura 1

1 Paulo mutume(si mutume kupitiya kwa wana damu, lakini kutoka kwa Yesu Kristo na Mungu Baba, mwenye alimufufula kutoka ku wafu) 2 pamoja na wandugu wenye wekonaishi na miye, kwa makanisa ya Galatia. 3 Neema na amani ikue kwenu kutoka kwa Mungu Baba wetu na Bwana Yesu Kristo, 4 mwenye alijitoa ye pekee ju ya ma zambi zetu, kusudi atuokowe ku wakati mubaya ihii tunaoishi, kufuatana na mapenzi ya Mungu na Baba yetu. 5 Sifa irudi kwake milele na milele. 6 Minashangaa sana kumyona, munaacha na upesi (araka) Mwenye alimiita kwa neema ya Kristo. Minamishangaa nyinyi kugewukiya(kufwata) enjili ingine. 7 Si kusema kama kuko enjili ingine, lakini kuko batu benye biko namivuruga(mitatiza), na kutaka kuharibisha enjili ya Kristo. 8 Lakini, ikiwe sisi, ao(wala) malaika wa mbingu, akijaribu kuwapasha enjili ingine tofauti (isiyoambatana) na hii tulimihubiri, alainiwe. 9 Kama vile tulisema mbele, mina rudilia tena : "alainiwe, yeyote mwenye atajaribu kuwafundisha ingine enjili tofauti na ile muliamini." 10 Sababu, sasa, hakikisho ya nani ninataka, ya wanadamu wala ya Mungu? Niko natafuta kufurahisha wana damu? Kama niko paka natafuta kupendeza wanadamu, sina mutumishi wa Kristo. 11 Kwani minataka mujuwe wandugu, ya kama habari njema yenye nilihubiri, hayitoke kwa batu ba bure ba dunia. 12 Sikuyipata wala kufundishwa kutokeya kwa mwana damu. Lakini ni kupitiya kwa ufunuo ya Bwana Yesu Kristo mwenyewe kwangu. 13 Mulisikia habari ya maisha nilikuaka nayo mu dini ya kiyahudi, gisi nilikua natesa na kusumbua sana kanisa la Mungu. 14 Nilikua naendelea sana mu kiyahudi kushinda (kupita) wengi wa majirani ya kabila yangu. Nilikua na bidi sana (juhudi kubwa sana) ju ya tabia (mila) ya bababa yangu. 15 Lakini, ilimupendeza Mungu kunichagua tokeya tumbo ya mama yangu. Aliniita kupitia neema yake. 16 kua kunitambulisha(kunifunuliya) Mtoto wake ndani yangu, kusudi nimutangaze ku wapagani. sikuuliza mpaka sasa ata muili wala damu. 17 Sikupande ku Yerusalemi kwa benye balinitanguliaka kuitua watume. Lakini, nilienda Arabia na nikarudia Dameski. 18 Na kiisha myaka tatu njo nika hika sasa Yerusaleme kusudi ni muone Petro, na nikabakia naye ya pata siku kumi na tano. 19 Lakini siku ona bengine bamitume, kama sio tu Yakobo ndugu yake na bwana. 20 Ile ni kweli nawaambia siku sema bongo. 21 Kisha nilienda mu majumbo za suria na silisia. 22 Makaniso za Bwana zenye zili kua kule Yudea hazi kuniju. 23 Balikwa na ni sitia kwa jina tu na byenye nilikuwaka na fanya baka kua na shangala, na kusema, ule mwenye alikuaka na tu tesa ju ya enjili, ye peke ana hubiri ile imani ye nye alikuaka na tafuta kuzuiya. 24 Maka nisa zilikua na shukuru Mungu.