Genesis 7
Genesis 7:1
Dume na jike saba wa aina gani ya wanyama walipaswa kuingia ndani ya safina?
Dume na jike saba wa kila mnyama safi na ndege walipaswa kuingia ndani ya safina.
Genesis 7:4
Mungu alisema mvua itaendelea juu ya nchi kwa muda gani?
Mungu alisema ya kwamba mvua itaendelea kwa siku arobaini za mchana na siku arobaini za usiku.
Genesis 7:6
Nuhu alikuwa na umri gani gharika lilipokuja juu ya nchi?
Nuhu alikuwa na umri wa miaka mia sita pale ambapo gharika lilikuja juu ya nchi.
Genesis 7:8
Nuhu aliwaletaje wanyama ndani ya safina?
Wanyama walikuja kwa Nuhu na kuingia ndani ya safina.
Genesis 7:11
Maji ya gharika yalitoka katika vyanzo gani viwili?
Maji yalitoka katika chemichemi zote za vilindi , na kutoka angani.
Genesis 7:15
Pale watu na wanyama walipokwisha ingia ndani ya safina, nani aliufunga mlango?
Yahwe aliufunga mlango nyuma yao.
Genesis 7:19
Maji yalipanda kimo gani juu ya nchi?
Maji yalipanda urefu wa dhiraa kumi na tano juu ya vilele vya milima.
Genesis 7:21
Nini kilikufa juu ya nchi kwa sababu ya gharika?
Viumbe wote waliotembea juu ya nchi, na wanadamu wote walikufa.
Genesis 7:23
Watu gani pekee ndio waliosalia juu ya nchi?
Nuhu pekee na wale waliokuwa naye ndani ya safina walibaki hai.